Image captionMfanyibiashara huyo aliyezaliwa mjini Glasgow, alifungua biashara yake mwaka wa 1954.
Bilionea muuza magari Arnold Clark, ambaye ni mwanzilishi wa kundi huru la kuuza magari nchini Uingereza amefariki akiwa na umri wa miaka 89.
Mfanyibiashara huyo aliyezaliwa mjini Glasgow, alifungua biashara yake mwaka wa 1954.
Taarifa ziliarifu kwamba alifariki kwa amani akiwa amezungukwa na familia yake.
Iliongezea kwamba Sir Arnold alikuwa mfano wa kuigwa na kwamba familia yake itaendelea kubeba maono yake.
Alidhibitishwa kama bilionea wa kwanza Uingereza aliyekuwa kwenye biashara za magari katika orodha ya matajiri katika gazeti la Sunday Times mwaka 2016.
Kampuni hiyo ambayo ina majina ya Sir Arnolds ina maduka 200 katika maeneo kadhaa Uingereza, ikiwa na zaidi ya magari 18,000 mapya na pia magari yaliotumika na kuwekeza faida ya puundi milioni 107.2 kwa mauzo ya paundi billioni 3.2
Taarifa kutoka kwa familia ilisema kuwa alifariki akiwa amezingirwa na familia.
Alikuwa bwana, baba na babu aliyependwa na rafiki mkubwa na mwajiri wa wengi.
Kampuni yake, Arnold Clark Automobiles, ilisema ilihuzunishwa kutangaza kifo cha mwanzilishi na mwenyekiti wake.
Image captionRoma Mkatoliki akizungumza na vyombo vya habari
Msanii Roma Mkatoliki asema anahofia maisha yake siku moja tu baada ya kupatikana katika kituo cha polisi cha Oysterbay.
Akizungumza na vyombo vya habari akiwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe, msanii huyo ameelezea vile walivyotekwa siku ya Jumatano na kufungwa pingu na kitambaa usoni na baadaye kusafirishwa hadi eneo wasilolijua.
Akizungumza na hisia na uchungu mwingi Roma alisema kuwa walipofikishwa walipopelekwa walipata mateso mengi kwa kupigwa hadi siku ya Ijumaa usiku.
Roma Mkatoliki: Tukatolewa tulimokuwepo siku ya ijumaa jioni na kufungwa uso, na mikono na miguu. Tukapelekwa sehemu tukatupwa kwenye dimbwi la maji karibu na baharini Roma anasema kuwa alipata fahamu na kuweza kuwafungua wenzake na kutembea mwendo mrefu ambapo walifika katika maeneo ya Ununio.
Hatahivyo msanii huyo alishindwa kuelezea baadhi ya maswali aliyoulizwa kuhusu mahojiano na waliowateka huku akisema tu kwamba tayari wamewasilisha malalmishi yao kwa polisi kwa uchunguzi.
Wasanii waomba usaidizi wa kumtafuta Roma Mkatoliki
Harakati za waandishi za kumtaka azungumze kuhusu mahojiano hayo ziligonga mwamba huku maafisa wa serikali walioandaa mazungumzo hayo na wanahabari wakimzuia msanii huyo kusema lolote .
Awali Roma na wenzake walionyesha baadhi ya majeraha waliyopata chini ya watu waliowateka na kusisitiza kwamba kile walichokipitia sio suala la mzaha.
Wameitaka serikali kuwahakikishia usalama wao wakidai kwamba licha ya kuwepo katika eneo lililozungukwa na watu maarufu ikiwemo serikalini watekaji wao walifanikiwa kutekeleza tendo hilo bila wasiwasi.
Image captionKombora la Korea Kaskazini, Tayari kufyatuliwa
Mataifa mawili ya bara Asia, yametoa onyo kali dhidi ya utawala wa Pyongyang, kwamba itaadhibiwa vikali, iwapo itadhubutu tena kufanyia majaribio zana zake za kinuklia.
Mataifa hayo, Korea Kusini na China, yamekiri kuchukua hatua kali dhidi ya Korea Kaskazini, ikiwa tena itafanyia majaribio zana zake za kitonoradi zinazovuka mipaka ya kimataifa.
Tangazo hilo linatukia baada ya mkutano uliofanyika Seoul, kati ya wajumbe wa China na Korea Kusini, na hatua ya Marekani ya kutumameli za kivita hadi katika maeneo ya maji kwenye rasi ya Korea.
Taifa la Korea Kaskazini mara kwa mara limekuwa likiimarisha uwezo wake wa kivita, licha ya kuwekewa vikwazo na Umoja wa mataifa.