Tuesday, March 28, 2017

Uwanja wa ndege waitwa jina la Ronaldo Ureno

Muonekano wa uwanja wa Madeira kwa sasa
Image captionMuonekano wa uwanja wa Madeira kwa sasa
Licha ya kupoteza 2-1 dhidi ya Sweden Ronaldo ataondoka kwa ufahari nchini mwake baada ya uwanja wa ndege wa Madeira sehemu aliyozaliwa kubadiliwha njina na kuwa uwanja wa ndege wa Cristiano Ronaldo
Ureno walianza kupata goli baada ya mlinzi wa Sweden Andreas Granqvist kujifunga mwenyewe dakika ya 71.
Viktor Claesson akaiandikia Sweden goli la kwanza kabla ya Cavaco Cancelo kujifunga muda wa majeruhi.
Ronaldo anatarajiwa kuhudhuria sherehe za kuitwa jina hilo siku ya Jumatano.
Ronaldo ni miongoni mwa wachezaji wenye historia ya kuvutia zaidi Ureno
Image captionRonaldo ni miongoni mwa wachezaji wenye historia ya kuvutia zaidi Ureno
Mchezaji huyo mwenye miaka 32 aliyeingoza timu yake ya taifa kutwaa kombe la mataifa ya Ulaya 2016, amezaliwa katika mji wa Madeira katika kitongoji cha Funchal, kabla ya kujiunga na timu ya Lisbon na baadaye Manchester United.
Baadhi ya wanasiasa wamepinga uamuzi wa kubadili jina la uwanja wa ndege wa Maderia kuitwa Cristiano Ronaldo Airport.

Sarafu ya dhahabu ya $4m yaibiwa Ujerumani

Vienna, AustriaHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionMfano wa sarafu iliyoibwa
Sarafu kubwa iliyotengenezwa kwa dhahabu, ambayo ina picha ya Malkia Elizabeth wa Uingereza, ambayo inakadiriwa kuwa na thamani ya $4m (£3.2m), imeibiwa kutoka kwenye makumbusho Ujerumani.
Sarafu hiyo kutoka Canada imeandikwa kuwa ya thamani ya $1m, lakini kwa sababu imetengenezwa kwa kilo 100 za dhahabu, thamani yake ni ya juu sana kwa kutumia bei ya sasa ya dhahabu.
Iliibiwa usiku kutoka makavazi ya Bode mjini Berlin.
Haijabainika ni vipi wezi walifanikiwa kuingia bila kugunduliwa na mtambo wa kuzuia wezi, na kisha wakafanikiwa kutoroka na sarafu hiyo ambayo nusu kipenyo chake ni cha nusu mita.
Wizi huo unaaminika kutekelezwa mwendo wa saa tisa unusu alfajiri Jumatatu.
Sarafu hiyo inadaiwa kuwa nzito sana kiasi kwamba mtu mmoja hawezi kuibeba.
Polisi wa eneo hilo wanasema huenda polisi waliingia kupitia dirisha.
Ngazi ilipatikana imetupwa kwenye reli iliyo karibu, msemaji wa polisi Winfrid Wenzel aliambia Reuters.
"Sarafu hiyo ilikuwa imehifadhiwa ndani ya sehemu isiyoweza kupenya risasi ndani ya makumbusho," alisema.
Sarafu hiyo ilifuliwa mwaka 2007 na Royal Canadian Mint.

Brexit: Uingereza yaanza rasmi kujiondoa EU

Theresa MayHaki miliki ya pichaPA
Image captionTheresa May akitia saini barua ya kuanza kujiondoa EU
Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May ametia saini barua ambayo itaanzisha rasmi mchakato wa kuiondoa Uingereza kutoka kwa Muungano wa Ulaya.
Barua hiyo inatoa taarifa rasmi ya kujiondoa kwa muungano huo kwa kitumia Kifungu 50 cha Mkataba wa Lisbon.
Itawasilishwa kwa rais wa Baraza la Ulaya Donald Tusk baadaye leo.
Kwenye taarifa kwa bunge la chini nchini Uingereza, Bi May baadaye anatarajiwa kuwaambia wabunge kwamba hatua hiyo inaashiria "wakati we taifa letu kuungana pamoja."
Hatua hiyo imechukuliwa kutokana na kura ya maoni iliyoandaliwa Juni mwaka jana, ambapo wapiga kura waliunga mkono kujiondoa kutoka kwa EU.
Barua ya Bi May itawasilishwa kwa Bw Tusk Jumatano mwenzo wa saa sita unusu adhuhuri saa za Uingereza na balozi wa nchi hiyo katika EU Sir Tim Barrow.
Waziri mkuu ambaye ataongoza kikao cha baraza la mawaziri asubuhi, baadaye atatoa hotuba rasmi kwa wabunge kuthibitisha kwamba mchakato wa Uingereza kujiondoa EU umeanza.
MaandamanoHaki miliki ya pichaEPA
Image captionBi May amewaomba watu walio Uingereza kuungana
Ataahidi "kuwakilisha kila mtu katika Uingereza yote" wakati wa mazungumzo hayo - wakiwemo raia wa EU (wanaoishi Uingereza), ambao bado haijafikiwa uamuzi kuhusu hatima yao baada ya Uingereza kujiondoa kutoka kwa muungano huo.
"Nimejitolea kuhakikisha tunapata mkataba bora zaidi kwa kila mtu katika nchi hii," anatarajiwa kusema.
"Kwani, tunapokabili fursa na changamoto zilizopo mbele yetu, maadili yetu ya pamoja, maslahi na ndoto zetu zinaweza - na ni lazima - zitulete pamoja."

Matukio makuu yanayotarajiwa

  • 29 Machi, 2017 - UIngereza yaanza kutumia Kifungu 50
  • 29 Aprili- Mkutano mkuu wa viongozi 27 wa EU (bila Uingereza) kuipa Tume ya Ulaya ruhusa ya kushauriana na Uingereza
  • Mei - Tume ya Ulaya kuchapisha mwongozo wa mashauriano kwa kufuata ruhusa kutoka kwa viongozi wa EU. EU inaweza kuzungumzia uwezekano wa mashauriano sambamba wa mkataba wa baadaye wa biashara kati ya UK na EU
  • Mei/Juni 2017 - Mashauriano kuanza
  • 23 Aprili na 7 Mei - Uchaguzi wa urais Ufaransa
  • 24 Septemba - Uchaguzi wa ubunge Ujerumani
  • Majira ya kipupwe 2017 - Serikali ya Uingereza inatarajiwa kutunga sheria ya kujiondoa EU na kuweka sheria zote zilizopo chini ya EU kuwa sehemu ya Sheria za Uingereza
  • Oktoba 2018 - Mashauriano yanatarajiwa kukamilika
  • Kati ya Oktoba 2018 na Machi 2019 - Mabunge ya Uingereza, baraza la Ulaya na Bunge la Ulaya kupigia kura mkataba utakaokuwa umeafikiwa
  • Machi 2019 - UK kujiondoa rasmi kutoka EU.

Thursday, March 23, 2017

Waziri aliyetimuliwa Tanzania amwagiwa sifa kiongozi wa chama cha upinzani

Nnape NauyeHaki miliki ya pichaNNAPE NAUYE/TWITTER
Kiongozi wa chama cha Alliance for Change & Transparency Wazalendo nchini Tanzania Zitto Kabwe amesema waziri wa habari aliyefutwa kazi Bw Nape Nnauye "ni shujaa".
Kwenye Twitter, Bw Kabwe, ambaye ni mbunge wa Kigoma-Ujiji Municipality amesema amewasiliana na Bw Nnauye ambaye amemthibitishia kwamba ni kweli ameondolewa kwenye wadhifa wake wa uwaziri.
Taarifa kutoka ikulu mapema leo ilitangaza waziri mpya wa habari, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kuwa Dkt. Harrison George Mwakyembe.
Taarifa hiyo haikusema chochote kuhusu hatima ya Bw Nnauye.
KabweHaki miliki ya pichaTWITTER
Dkt Mwakyembe amekuwa akihudumu kama Waziri wa Katiba na Sheria.
Bw Nnauye kwenye Twitter amewaomba watu kuwa na subira na kuahidi kwamba atazungumza na wanahabari baadaye leo.
"Ndugu zangu naomba TUTULIE! LEO mchana nitakutana na Wanahabari na tutalizungumza hili. Nitawaambia saa na mahali, kwasasa naomba TUTULIE!" ameandika.


Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF) limempongeza Dkt Mwakwembe kufuatia uteuzi wake.

Magufuli ateua waziri mpya wa habari Tanzania, amvua uwaziri Nnauye

Rais MagufuliHaki miliki ya pichaIKULU, TANZANIA
Image captionRais Magufuli
Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli amefanya mabadiliko madogo katika Baraza la Mawaziri na kumteua waziri mpya wa habari na michezo.
Dkt. Magufuli amemteua Dkt. Harrison George Mwakyembe kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.
Bw Nape Moses Nnauye ndiye aliyekuwa anashikilia wadhifa huo.
Aidha, Dkt Magufuli amemteua Prof Palamagamba Aidan John Mwaluko Kabudi kuwa Waziri wa Katiba na Sheria.
Dkt Mwakyembe amekuwa akihudumu kama Waziri wa Katiba na Sheria.
"Uteuzi huu unaanza mara moja," taarifa kutoka ikulu imesema.
Wateule wote wataapishwa Alhamisi kwa mujibu wa ikulu.
Bw Nauye amevuliwa majukumu yake siku moja baada yake kupokea ripoti ya kamati ya uchunguzi kuhusu uvamizi uliotekelezwa na mtu anayedaiwa kuwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda katika studio za kituo cha habari cha kibinafsi cha Clouds mwishoni mwa wiki.
Waziri wa zamani wa habari aliyevuliwa madaraka Nape Nnauye
Image captionWaziri wa zamani wa habari aliyevuliwa madaraka Nape Nnauye
Kamati hiyo, kwenye ripoti yake, ilionekana kumkosoa Bw Makonda na kusema alitumia vibaya mamlaka yake.
Kamati hiyo ilipendekeza, miongoni mwa mengine, kwamba Bw Nnauye awasilishe malalamiko ya waandishi wa habari dhidi ya mkuu huyo wa mkoa kwa Rais wa Tanzania pamoja na kuanzishwa kwa uchunguzi dhidi ya polisi waliongia na silaha za moto kwenye chombo hicho cha utangazaji.
Akipokea ripoti hiyo, Bw Nnauye pamoja na kuwataka viongozi wa umma kufanya kazi kwa uweledi, aliahidi kukabidhi taarifa hiyo kwa mamlaka za juu zaidi ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa kutokana na mapendekezo yaliyomo katika taarifa hiyo.
Dkt Magufuli ameonekana kufurahishwa na utendakazi wa Bw Makonda na mara kwa mara amesifu hatua alizochukua.
Rais John Magufuli alisema katika hotuba yake Jumatatu alipokuwa akizindua ujenzi wa barabara ya juu eneo la Ubungo, jijini Dar es Salaam kuwa Bw Makonda aendelee kuchapa kazi na kwamba yeye hafanyii kazi maneno ya kwenye mitandao kwa sababu yeye ndiye rais wa nchi.
Dkt. Harrison George Mwakyembe awali alikuwa waziri wa sheria sasa ni waziri wa habari
Image captionDkt. Harrison George Mwakyembe awali alikuwa waziri wa sheria sasa ni waziri wa habari
Dkt Magufuli alisema kuwa kuna baadhi ya watu wanaingilia majukumu yake wakati yeye ndiye mwenye uamuzi na kwamba hapangiwi kazi ya kufanya kwa sababu anajiamini.
Prof Kabudi, ambaye ameteuliwa kuwa waziri mpya wa katiba na sheria aliteuliwa Januari mwaka huu kuwa mbunge mteule.
Awali Prof. Palamagamba Aidan Kabudi alikuwa mhadhiri wa chuo kukuu cha Dar es salaam na sasa ameteuliwa kuwa waziri wa sheria
Image captionAwali Prof. Palamagamba Aidan Kabudi alikuwa mhadhiri wa chuo kukuu cha Dar es salaam na sasa ameteuliwa kuwa waziri wa sheria
Yeye ni mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Kitivo cha Sheria na alikuwa mmoja kati ya wajumbe wa Tume ya Kukusanya na Kuratibu Maoni ya Katiba, iliyokuwa chini ya uenyekiti wa Jaji Mstaafu Joseph Warioba.

Tuesday, March 14, 2017

Mgombea urais nchini Ufaransa kuchunguzwa

Francois FillonHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionFrancois Fillon
Mgombea kiti cha urais nchini Ufaransa Francois Fillon, sasa anachunguzwa rasmi kwa tuhuma kwamba alimfanyia mipango mkewe muingereza, alipwe mshahara kwa kazi ya usaidzi katika bunge.
Fillon anakana madai hayo na kudai ataendelea na kampeni za uchaguzi huo wa mwezi ujao.
Bwana Fillon anadaiwa kumlipa mkewe na wanawe wawili kazi iliyokuw ifanywe bungeni lakini haikufanywa madai ambayo wote wanakanusha.
Wakati mmoja Fillon alisema kwamba atajiuzulu kama mgombea wa chama cha Republican iwapo atachunguzwa rasmi lakini baadaye alibadili msimamo huo.
Anasema kuwa atakabiliana na kile anachokitaja kuwa vita vya kisiasa.
Hadi hivi majuzi alionekana kama mgombea bora kwenye uchaguzi ambao utaandaliwa Aprili na Mei.


Lakini waziri huyo mkuu wa zamani anaonekana kuteleza na kujipata nyuma ya mgombea wa chama cha National Front, Marine Le Pe na Emmanuel Macron.

Mgombea urais nchini Ufaransa kuchunguzwa

Francois FillonHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionFrancois Fillon
Mgombea kiti cha urais nchini Ufaransa Francois Fillon, sasa anachunguzwa rasmi kwa tuhuma kwamba alimfanyia mipango mkewe muingereza, alipwe mshahara kwa kazi ya usaidzi katika bunge.
Fillon anakana madai hayo na kudai ataendelea na kampeni za uchaguzi huo wa mwezi ujao.
Bwana Fillon anadaiwa kumlipa mkewe na wanawe wawili kazi iliyokuw ifanywe bungeni lakini haikufanywa madai ambayo wote wanakanusha.
Wakati mmoja Fillon alisema kwamba atajiuzulu kama mgombea wa chama cha Republican iwapo atachunguzwa rasmi lakini baadaye alibadili msimamo huo.
Anasema kuwa atakabiliana na kile anachokitaja kuwa vita vya kisiasa.
Hadi hivi majuzi alionekana kama mgombea bora kwenye uchaguzi ambao utaandaliwa Aprili na Mei.


Lakini waziri huyo mkuu wa zamani anaonekana kuteleza na kujipata nyuma ya mgombea wa chama cha National Front, Marine Le Pe na Emmanuel Macron.